Na C-Sema
Katika dunia inayobadilika kila siku, usalama wa wasichana unazidi kuwa suala la msingi kwa wazazi na jamii kwa ujumla. Miongoni mwa changamoto kubwa za vitendo vya ukatili wa kijinsia vinavyowakumba zinazowakumba mabinti zetu ni ukatili wa kijinsia (GBV), ambao hujumuisha vitendo vya unyanyasaji wa kimwili, kingono, kihisia, ndoa za utotoni na ukeketaji (FGM).
Wiki hii tuliadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kupinga Ukeketaji wa Wanawake na Wasichana (Februari 6), hivyo, ni muhimu kujadili njia bora za kuwalinda mabinti dhidi ya vitendo hivi vinavyovunja haki zao za msingi.
Kwa mujibu wa Taarifa ya Utafiti wa Afya na Uzazi wa Mtoto na Viashiria vya Malaria (TDHS-MIS) 2022/23, kiwango cha ukeketaji kwa wasichana wa umri wa miaka 15-49 nchini Tanzania kimeshuka hadi asilimia nane kutoka asilimia 10 mwaka 2015/16.
Soma https://thechanzo.com/2025/02/11/usalama-wa-mtoto-wa-kike-dhidi-ya-ukatili-wa-kinjinsia-ni-jukumu-la-nani/