وَذَكَرَ الْخَطِيبُ الْحَافِظُ أَنَّهُ مَذْهَبُ الْأَئِمَّةِ مِنْ حُفَّاظِ الْحَدِيثِ وَنُقَّادِهِ مِثْلِ الْبُخَارِيِّ، وَمُسْلِمٍ، وَغَيْرِهِمَا.
Na ama Jarhu basi kwa hakika haikubaliwi isipokuwa (ikiwa) imefasiriwa na imebainishwa sababu, kwasababu watu wanatofautiana katika lile ambalo linajeruhi na lile ambalo halijeruhi, basi (akatamka) kwa kuachia mmoja wao Jarhu kwa kuijengea juu ya jambo analiitakidi ni Jarhu na (kumbe) si Jarhu katika jambo hilo hilo, basi haina budi Ubainifu (kubainisha) sababu yake, ili itazamwe ndani yake; Je, ni Jarhu au sio(Jarhu), na hii iko wazi na ni utajo-unaokiriwa katika Fiqhi na Msingi yake.
Na ametaja Al-Khatwiybu Al-Haafidhw kwamba (hiyo ni) Madh'habu ya Maimamu katika Waliohifadhi Hadiyth na Wakosoaji wake mfano Al-Bukhaariy na Muslim na wengine.
(Rejea: imenukuliwa kutoka katika tovuti ya Ashaykh Ar-Raajihiy حفظه الله تعالى, itafuata utajo wake katika rejea ya Sharhu).
Amesema Ashaykh Mwanachuoni 'Abdul'Aziyz bn 'AbdiLlaah Ar-Raajihiy (حفظه الله تعالى) akisherehesha maneno hayo:
الجرح لا بد أن يبين السبب، فإذا قال المحدث أن هذا الراوي غير عدل مجروح، ما يقبل حتى يبين، مجروح لأنه مثلًا يفعل كذا من الفسق، يفعل كذا، يشرب الخمر، يذكر السبب حتى ينظر، لأن بعضهم قد يعده جرح وهو ليس بجرح، قد يقول مجروح، فإذا قيل له لماذا؟ قال رأيته يأكل في الشارع مثلًا، هذا قد يكون مخارم المروءة، وقد يكون في بعض الأحيان أنه لا بأس بالأكل في بعض الأزمنة، يأكل في مطعم مثلًا، فلا بأس في هذا، فقد يجرح بعض عوام الناس فيقول رأيته يأكل في مطعم فهذا يعتبر جرح، نقول هذا ما هو ليس بجرح، لا بد يبين، الجرح لا بد أن يبين..
Jarhu haina budi ibainishwe sababu, basi akisema Mtu wa Hadiyth kwamba huyu mpokezi si muadilifu (ni) aliyejeruhiwa, haikubaliwi mpaka ibainishwe, (ni) aliyejeruhiwa kwasababu yeye mfano anafanya kadha katika ufasiki, anafanya kadha, anakunywa pombe(ulevi), anataja sababu mpaka itazamwe, kwasababu baadhi yao anaweza akaihesabu ni Jarhu na (kumbe) sio Jarhu, anaweza akasema (ni) aliyejeruhiwa, ikisemwa kuambiwa yeye, "kwasababu gani?" Akisema nimemuona akila njiani mathalani, hii ni inakuwa katika viondoshaji murua, na inakuwa katika baadhi ya wakati hakuna tatizo, kwa kula katika baadhi ya zama, anakula katika mgahawa mathalani, hakuna tatizo katika hili, basi anaweza akajeruhi baadhi ya(mtu)katika Maawam, basi akasema, "nimemuona anakula mgahawani, basi hii izingatiwe ni Jarhu, tunasema hii sio Jarhu, haina budi ibainishwe; Jarhu haina budi (isipokuwa) ibainishwe...
(Rejea, tovuti ya Ashaykh katika kiungo https://shrajhi.com.sa/lessons/1234 ).
Nasema: Hilo linajulisha yale tuliyotanguliza kwamba kuna wakati mtu anaweza kutumia neno ambalo ni Jarhu lakini juu ya jambo hilo mtu hapaswi kujeruhiwa kwalo.
Na hili ndilo lililotokea kwa hawa ambao wanasema kuwa wanaofanya Tarjama ni watovu wa adabu.
Kisha wale wenye kuchukua kauli kwasababu tu Al-Ustaadh Abuu Usaamah Khamis amesema hawakutazama ni kwa Wajihi gani kinachofanyika ni utovu wa adabu na ni ipi dalili, lakini wao wakaelekea katika kubeba maneno hayo kibubusa.
Hivyo basi inatakiwa watu wachunguze wasikurupuke, wajue kabisa ni kwa dalili ipi kufanya Tarjama ya Ruduud za Kielimu zilizotiwa nguvu kwa dalili za kisheria ni utovu wa adabu.
Na tayari tulikwisha bainisha Uhalisia wa ufanyaji wa Tarjama wa Ruduud za Ashaykh Az-Za'iym (حفظه الله تعالى) Kwa ndugu 'Adnaan Al-Maswqariy, kwamba ni katika kuondoa munkar tena kwa njia ya kisheria na Mwenendo wa kisheria.
Basi ni juu yenu mthibitishe kuwa ni jambo baya kwa dalili za kisheria ili Jarhu yenu iwe imefungamana na dalili, hilo la kwanza katika sura hiyo.
Ama ikiwa ni kwasababu hoja yenu, ni kwasababu Shaykh Saliym Al-Hilaaliy (حفظه الله تعالى) amesema kama mnavyonukuu (na itakuja majibu zaidi In Shaa Allaah) iko wapi dalili yenu kwamba kumukhalifu katika hili ni utovu wa adabu?
Lakini ikiwa kauli yenu ni hatakiwi kukhalifiwa kwenye jambo lolote basi itatushangaza kwani itakuwa ndio ile ile kauli ya Masuwfiy. Na kujikinga ni kwa Allaah.