Chakushangaza (@chakushangaza) के नवीनतम पोस्ट टेलीग्राम पर

Chakushangaza टेलीग्राम पोस्ट

Chakushangaza
Njoo▶tukujuze ▶tukushangaze ▶tukuelimishe ▶tuulishe ubongo wako madini

CHANNEL ILIANZISHWA RASMI MNAMO 11/06/2019
4,721 सदस्य
4,984 तस्वीरें
168 वीडियो
अंतिम अपडेट 28.02.2025 22:03

समान चैनल

MILLARD AYO NEWS
1,615 सदस्य
COMPUTER FILES 🇰🇪
1,180 सदस्य

Chakushangaza द्वारा टेलीग्राम पर साझा की गई नवीनतम सामग्री


(SEHEMU YA KWANZA)

UVUNJAJI NA UWIZI NDANI YA BOHARI SALAMA {SAFE DEPOSIT} YA HATTON GARDEN

Tumewahi kusikia, kuona au kusoma kuhusu uvunjaji na uwizi katika mabenki, mabohari salama au magari ya kubebea fedha katika sehemu mbalimbali duniani lakini wafanyaji matukio mara zote tumeshuhudia wakiwa ni vijana wanaotafuta pa kutokea katika maisha ila kwa makala yetu ya leo tunaenda kuona wazee ambao wengi wetu huwa tunawadharau na kuwaona wameshachoka kimwili na kiakili ila kwa wazee hawa al maarufu kwa jina la ‘THE GRANDPA GANG’ nafikiri wengi wetu watatubadilisha mtazamo wetu wa siku zote kwa wazee, kwani walichofanya ni zaidi ya kijana angefanya.
Mimi ningependa kuwaita wazee katika ubora wao kwa namna walivyochekecha akili zao na kuweza kustaajabisha dunia na kuweza kuweka rekodi ndani ya nchi ya uingereza katika jiji kubwa lenye ulinzi mkali la LONDON kwa kuweza kuiba katika bohari salama yenye ulinzi mkali vitu vyenye thamani kubwa katika historia ya nchi ya uingereza tangu dunia ianzishwe bila kutumia silaha yoyote zaidi ya akili kubwa na ueledi uliotukuka katika Nyanja za uwizi. Na hapa ndo msemo wa ‘uzee mwisho chalinze’ ndipo unapotimia kupitia wazee wetu hawa tutakaoenda kuwaona. Ni uwizi wa aina yake uliostaajabisha watu na sio kwasababu ya mali nyingi zilizoibiwa ila ni watu walioiba (wazee), njia iliyotumika kuiba na muda wa uwizi ulivyopangwa kwani ni moja ya uwizi uliotumia muda mrefu katika upangaji wake ambao ni miaka mitatu ambayo kiukweli inataka subira kwa wale wenye harakaharaka ila kwa hawa wazee walisimama na msemo "SUBIRA YAVUTA HERI". TUKIO ZIMA

Katika mpango wa tukio hili la uwizi lilijumuisha wazee wezi nane ambao walijikusanya na kuunda kundi lililoitwa ‘THE GRAND PA GANG’ likiwa na dhumuni kuu la kufanya uhalifu utakaocha historia nchini uingereza na kuongelewa duniani kote kutokana na ufundi utakaotumika kwenye uwizi wao.

Hawa wazee wanajulikana kwa majina ya KENNY COLLINS (75), DANIEL JONES (61), TERRY PERKINS (67), CARL WOOD (59), WILLIAM LINCOLN (60), HUGH DOYLE (50). BRIAN READER (76) na MR.BASIL [huyu nitakuja kumuelezea kwanini hajulikani jina lake halisi wala umri wake kama wenzake]. INAENDELEA...!!!

#CHAKUSHANGAZA
ASILI YA JINA CHERAHANI YA KUSHONA NGUO.
Mwaka 1890 Charan Singh alikuwa mhindi wa kwanza kufika Kisumu nchini Kenya na kuanzia kutumia mashine hiyo ya kushona nguo, na Kwa kuwa jina lake aliitwa Charan, watu wakatumia jina lake hilo kuiita mashine hiyo kuwa ni CHERAHANI.
Ninaimani umeelimika.

#CHAKUSHANGAZA
SIKU UNCLE TOM ALIPOTAKA KUIPINDUA SERIKALI YA MWALIMU NYERERE, HAKIKA CHA MOTO ALIKIPATA.

Uvumi huo mitaani ulikuja kuwekwa hadharani baada ya magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Daily News, kuandika kwa ufupi sana hivyo Wengi wakafahamu juu ya tukio hilo. Ikasemekana kiongozi wa jaribio hilo ni Pius Mutakubwa Lugangila, ambaye alitokea Uingereza na alijulikana kama Father Tom au Uncle Tom, Uncle Tom alitamani sana kuwa Rais hivyo akapanga mpango huo wa kumwondoa Ikulu Mwl Nyerere,kipindi hicho Uncle Tom alikuwa na pesa za kutosha, nyingi, na alikuwa akiishi London, Uingereza, wakati huo Uncle Tom alikuwa na undugu na Christopher Pastor Ngaiza ,aliyekuwa mtumishi wa Serikali ofisi ya Rais Ikulu.

Inasemekana Uncle Tom alimwita Ngaiza ambaye ni Mjomba wake, wakati huo Ngaiza alikuwa London Uingereza, akakutana na mpwa wake huyo ambaye ni Uncle Tom, " Mjomba ,hivi mimi nikitaka kuwa Rais wa Tanzania nifanyeje?" Aliuliza uncle Tom. Ngaiza alimjibu mpwae kuwa kuna namna mbili tu, akamwambia kuna kupitia njia ya Demokrasia, Ingawa hiyo ni njia ngumu au kupitia Mapinduzi ya kijeshi ,hii ya pili ilionekana ni Jibu la utani tu, lakini uncle Tom akalichukua na kuanza kulifanyia kazi.

Toka hapo Uncle Tom akafunga safari kutoka London Uingereza na kuelekea Dar es salaam, alipofika akakutana na Maximilian Rugaimukamu, ambaye alikuwa ni Raia wa kawaida na ni miongoni mwa raia waliokuwemo kwenye kesi ya uhaini baada ya jaribio la Mapinduzi kufeli. Kipindi hicho hapo Dar es salaam Rugaimukamu alikuwa ndio mmoja wa watoto wa mjini ,na alikuwa akishinda sana maeneo ya Market Street, hapo kilikuwa ndio kijiwe chake. Rugaimukamu alikuwa ndio kiunganishi cha mawasiliano kati yake uncle tom na wadau Wengine waliotakiwa kutekeleza tukio hilo wakiwemo wanajeshi Vijana.

Miongoni mwa watu wa mwanzo ambao uncle tom aliwapata ni Kapteni Badru Rwechungura Kajaja, huyu alifanya kazi ya kuwatafuta wanajeshi Wengine baada ya kuahidiwa pesa ndefu na uncle tom, wa kumaliza kazi iliyokuwa usoni mwao,na Wengine walikuwa na vyeo vya kuanzia Kapteni kushuka chini ,wakaingia wengi kama Luteni Eugene Maganga, Kapteni Vitalis Mapunda, Kapteni Mbogoro, Kapteni mkude ,kapteni Albert Barati,( Kamisheni ya Zanzibar) Kapteni Rodrick Rosheni Robert, Kapteni Zakaria Hanspope, Kapteni Methusela Komandoo, Komandoo Mohammed Mussa,(Martin Tamim) Kapteni Hatib Ghandi au Hatty McGhee nk.

Mikutano yote ilifanyika Kinondoni kwa Bwana mmoja aliyeitwa ,George Banyikwa, baada ya kujitolea nyumba yake kama sehemu ya kukutanikia ,kupanga mipango ya Mapinduzi ya kumng'oa Rais Julius Nyerere madarakani. Wakati wote wa vikao pale Kinondoni kapteni Hatibu Gandhi ( hakuwa mwanajeshi bali rubani wa ndege ndogo) alikuwa ndio amerudi toka uarabuni kwenye ukandarasi wa urubani na aliwadanganya wenzake kwamba yeye ni mwanajeshi wa majini wa Marekani, pia aliwatajia jina kwamba yeye anaitwa Hatty McGhee na walimjua hivyo siku zote katika vikao vyao ,alikuja kujulikana jina lake la Hatibu Gandhi wakati wa kesi yao ya uhaini kuanza Mahakamani, Hatty McGee alikuwa na Maneno mengi sana na mjanja mjanja.

Wakati mwingi Hatty McGhee alikuwa akiitumia Taxi ya kijana mmoja ambaye alikuwa anamleta na kumsubiria pale kwa masaa mengi na kijana yule alikubali kumsubiri kwasababu alikuwa analipwa pesa ya kutosha. Katika vikao hivyo palikuwa na mazungumzo yaliyoambatana na Bia na vinywaji vikali vya kutosha, Lugangila alikuwa na pesa nyingi na akawa anautamani Urais amwondoshe Ikulu Mwl Nyerere, yule dereva Taxi wa Hatty McGhee alikuwa akisikia mazungumzo yao wanapokuwa vikaoni ,akaenda kwa rafiki yake mmoja mwandishi wa Gazeti la Serikali la Daily News.

Kijana huyo wa Taxi ndiye aliyepata taarifa hizo za Mapinduzi ya kijeshi Kabla hata ya Serikali kujua kinachoendelea la isivyo Mapinduzi yangefanyika na kuondosha amani tuliyonayo leo. Baada ya kupata habari hizo toka kwa dereva wa Taxi, Mwandishi wa gazeti la Serikali la Daily News, alizipeleka kwa Naibu Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa Balozi Mahiga, akaamua kufanya uchunguzi ili kubaini kama kweli kulikuwa na mpango wa kutaka kupindua Serikali.

Kabla ya kushikwa wote na kuswekwa korokoroni kuna ijumaa moja tar 7 januari mwaka 1983 saa 9:30 mchana, Siku hii walipanga kuonana kwenye nyumba ile ile ya George Banyikwa karibu na Drive-Inn, siku hii walitakiwa wapewe taarifa kamili kwasababu Mapinduzi yalipaswa yafanyike Usiku uliofuata ,wakati huo walikuwa wameahirisha mara mbili baada ya Kiongozi wao uncle tom kuomba hivyo, ambaye ndiye mratibu, Uncle Tom akidai kwamba alikuwa anategemea meli zije na bidhaa muhimu kama dawa za meno, sabuni ,sukari nk.ili Mapinduzi yakifanyika awamwagie bidhaa hizo wananchi wote.

Kwanza walipanga Mapinduzi yafanyike Siku ya jumatatu, wakaahirisha mpaka jumatano, uncle Tom akadai tena hayuko tayari ikapigwa tena tarehe ya Juma lingine ,wale wanajeshi wakamuonya uncle tom na kumtahadharisha kwamba watu wengi wanahusika katika tukio lile hivyo ni hatari kwani taarifa zitavuja. Wanajeshi wale walikuwa hawafahamu kwamba uncle Tom ili kufanikisha tukio lile alikuwa pia anakwenda kwa Sangoma ( mganga wa kienyeji) kuweka mambo sawa kwa kupitia vibuyu na ndumba, akiwa na wenzake Komandoo Mohamed Tamimu na Hatty McGhee, walimtembelea sangoma huyo kujua siku ya bahati ya kumaliza kazi hiyo bila vikwazo vyovyote.

NI DOSSA AZIZ ALIYEMWOMBA MWALIMU NYERERE KUACHA TENA KUVAA KAPTULA MBELE YA WAZEE.

Aziz Ali Dossa Kidonyo, mmoja wa Waafrika matajiri wakati wa ukoloni nchini Tanganyika. Aziz Ali alijitengenezea umaarufu Kutokana na kwamba aliweza kumiliki majumba mengi na magari ya biashara ( yaani malori ya mchanga) pamoja na ya kutembelea na vitu vingine kadhaa, kutokana na kazi yake ya kuwa mtaalamu wa kujenga ( Building Contractor).

Hili jina la Aziz Ali alipewa na watu wa Dar es salaam kwa hisani na wema wake ,alikuwa ni tajiri na Contractor wa kujenga nyumba na mwafrika wa kwanza kununua magari na kujenga nyumba ya vigae na vioo mtoni. Aziz Ali alikuwa ni mdigo aliyetokea sehemu za Tanga na kuja kuweka kambi mjini Mzizima ( sasa Dar es salaam) mwanzo wa vita kuu ya kwanza ya dunia (1914--1918) akiwa askari katika jeshi la wajerumani na baada ya vita aliajiriwa na Goa mmoja.

Mwajiri wake huyo alipoondoka nchini alimwachia Aziz Ali gari mbili na hizi ndizo alizoanzia kufanyia biashara hapo mwanzo na kufungua kampuni ya ujenzi na kuajiri Mafundi kadhaa. Mwezi wa Ramadhani milango ya nyumba yake ilikuwa wazi kuwahudumia kwa futari mamia ya watu, Temeke imehifadhi jina lake kwa eneo moja la "Mtoni kwa Aziz Ali).

Kwenye Nyumba zake alikuwa akitoa fursa kwa watu kumpa pesa kidogo kidogo kama malipo ya nyumba alizokuwa anawajengea na alikuwa mtu akishindwa kulipa alimpa muda hadi atakapoweza ,Nyumbani kwake mwezi mtukufu wa Ramadhani alikuwa akitandika majamvi nje na kufuturisha hadi watu 100 asiowajua wakija wanafuturu na kuondoka.

Nyumba hii hadi leo ipo na sehemu hiyo kando kando ya barabara ya Kilwa na ndipo hapo pakaja kuitwa Mtoni kwa Aziz Ali. 🙏

#CHAKUSHANGAZA
Tukio hili lilitokea Januari 25, 1995 nchini Uingereza. Ni miaka 30 kamili sasa. Wangapi wanalikumbuka?

Eric Cantona alimpiga teke la flying kick shabiki aliyekuwa akitolea maneno machafu kila alipogusa mpira!

#CHAKUSHANGAZA
1970's Mwalimu Nyerere aliwahi Kumwambia Waziri wake Mkuu Hayat Mzee Rashid Kawawa kwamba "Umefanya Kazi Nzuri sana, sasa naomba nikupumzishe na nimpe Uwaziri Mkuu Sokoine, huyu Kijana nataka aendelee na Kazi kutoka ulipoishia, kuna jukumu nataka nimpe"

Ndipo kijana Jasiri toka Umasaini -Monduli kwa jina la Moringe Sokoine Akaingia kazini 13 February Mwaka 1977 na akaanza kutekeleza jukumu alilopewa, la kupambana na Wahujumu wa Uchumi, Vibaka,Walanguzi na Vibaraka.

Ndio!Hayati Moringe aliwanyoosha,na Ilipofika ule Mwezi wa November 1980 Baba wa Taifa akamuita Sokoine akamwambia Hakika Wewe Ni Mzalendo na Umefanya Kazi Kubwa Sana katika Miaka 3 na Sasa nakupeleka kusoma Nje Miaka 3 ili kuongeza Maarifa zaidi.

na Ndipo Sokoine akaenda Nje kusoma Zaidi kuhusu Uongozi na akampisha Cleopa Msuya aendee mpaka Mwaka 1983 ambapo Sokoine alirudi nchini na kurejeshwa tena ktk Uwaziri Mkuu Mpaka Mungu alipomchukua April 12, 1984 kwa ajali ya Gari..yaani kugongwa katikati ya Msafara, Ajali Fulani ya Kushangaza.

Ule Mwaka 1984 ambao Moringe Alifariki ndio Mwaka ambao Baba wa Taifa alitangaza kuwa Mwaka unaofuata 1985 atang'atuka Katika kiti Cha Urais, Mwalimu alimuona Sokoine Kama Mtu Sahihi Sana, Je Pengine aliona ndiye wa kuvaa Viatu Vyake na Sasa apumzike? na Sasa akaona Ni wakati Sahihi yeye kungatuka.Yes Ni ishara tosha, Maana Moja ya Sifa Kuu ambazo Mwalimu ali-share na Hayati Sokoine Ni ule Uchungu na Uzalendo wa Nchi katika kuchukia Rushwa na Kujilimbikizia Mali za Umma", Vita ambayo Sokoine alipambana nayo Mpaka Mauti yake, Hii ni Sifa ambayo Wanasiasa wengi wa "Tumbo Mbele" Hawana.

inaudhi, Tazama Leo, Mazingira ya Mtanzania wa kawaida kushiriki siasa yamefanywa kuwa magumu mno, Mara Nyingi wenye sifa na vipaji vya uongozi huwa hawapati nafasi za kushiriki uongozi kwa vile tu hawana fedha mifukoni au watu wa kuwafadhili.....Hivyo wale watu wasio na maadili na miiko ya uongozi hutumia fursa hiyo kuununua uongozi aidha kwa fedha zao au za wafadhili wao ambao watawarudishia fadhila mara tu baada ya kutwaa madaraka"

Na ikitokea Mtu Yeyote mwenye sifa,Maadili na Uzalendo akafanikiwa kupenya na kuchomoza katikati ya kundi la wale Wasio na Sifa na kushika hatamu ya Uongozi basi wale Wasio na Sifa huungana kupiga Vita na kuhujumu.

Mwalimu Nyerere Aliwahi kutamka Kwamba "Bila Nchi kupanga na kusimamia uchumi wake yenyewe na kwa Uaminifu basi kungeruhusu mamlaka za serikali kunyakuliwa, kutumikia, kunufaisha na kulinda matakwa ya kikundi kidogo kwa “maangamizi” dhidi ya Mwananchi wa Kawaida....na Vikundi Hivyo ni vya kuogopa Kama Ugonjwa wa Ukoma!

Credit to Pio Pius.🇹🇿


Channel name @Chakushangaza
Channel link t.me/chakushangaza


SAMBAZA MARA NYINGI UWEZAVYO

🗣️ Mwezini kunakwenda kuwa sehemu ya pili ambayo viumbe binadamu watakuwa wakipatikana ambapo mipango mikubwa ya mwanadamu ni kwenda kuanzisha makazi ya kudumu Mwezini .

— Haitakuwa jambo geni kwakuwa kwa mwaka 1969 Neil Amstrong alikuwa mwanadamu wa kwanza kabisa kukanyaga uso wa Mwezi akifatiwa na Buzz Aldrin ambaye yeye alikuwa mwanadamu wa pili kufanya hivyo kupitia misheni ya Apollo 11 .

— Adhimio la mwanadamu ni kutawanya uwepo wake katika eneo zaidi ya moja hapa ulimwenguni na kumfanya mwanadamu ni (multi planetary species) ambapo mpaka sasa bado hatujui kama kun viumbe wengine kama sisi katika eneo lolote lile hapa ulimwenguni .

— Mataifa mengi yamedhamiria kuhakikisha jambo hili linafanikiwa ambapo baadhi ya mataifa ni kama Marekani, China, Urusi, UAE Saudi Arabia, Umoja wa Ulaya na mengineyo .

— Awali hii safari za Mwezini zitakuwa za aina yake ambapo kwakuwa wanadamu watakaofila mwezini kwa mara hii hawataweza kurudi kwa kipindi kirefu bali watakuwa na kazi kubwa ya kuanzisha makazi madogo ya wao kuweza kuishi na kufanya chunguzi mbalimbali .

— Kumbuka mwezini ndio kutakapotumika kama kituo kikubwa cha kuanzisha safari za Sayari ya Mars hapo baadae ambapo kutakuwa na urahisi mkubwa kwa chombo kuliko kuanzishia safari za Mars kutokea duniani .

#AstronomyKiswahili

🗣️ Harakati za mwanzo kabisa za Umoja wa Kisoviet kuhakikisha wanapeleka mwanadamu anga za juu huku kuhakikisha usalama wa uhai wake,
Basi waliamua kumtumia Mbwa kwa majaribio ya kwanza kabisa ili waweze kufahamu ni kwa namna gani ataweza kuhimili hali ya mazingira ya anga za juu .

— Kutokea Moscow alichaguliwa Mbwa aliyeitwa Laika kwa ajili ya misheni hiyo mwaka 1957 ambapo alipandishwa katika chombo cha Sputnik 2 kwenda anga za juu kwa jambo la kuzunguka dunia .

— Masaa machache baada ya kurushwa kwa chombo hicho anga za juu Mbwa Laika alipoteza maisha kutokana na mazingira kadhaa ya anga za juu na kufuatiwa kuwa chombo kilikosa mazingira mazuri ya kukinga abiria ambaye alikuwa mbwa Laika yote ni kutokana na kukosa taarifa kamili ya yaliyopo katika safari nzima kuelekea anga za juu .

— Mbwa Laika anabaki kuwa kiumbe hai bora ambaye alifungua njia katika suala zima la viumbe hai kulitawala anga la juu la dunia yetu .

— Mpaka kufikia hatua hii ya sasa ya kupeleka wanaanga anga za juu basi fahamu kuna viumbe vingi vilitolewa kafara kuhakikisha mwanadamu anafanikisha jambo kubwa la kwenda anga za juu na kurudi salama .

#AstronomyKiswahili

🗣️ 25/01/2025 Sayari 6 zitaonekana angani kwa pamoja katika tukio la kiastronomia linalojulikana kama (Planetary Alignment) ambapo watu wa maeneo yote duniani wataweza kushuhudia mpangilio wa sayari hizi katika anga zao .

— Sayari zitakazoweza kuonekana angani ni kama Mars, Jupiter, Uranius, Neptune Venus na Saturn , lakini kwa macho ya kawaida utaweza kuona sayari 4 tu ambazo ni Mars , Jupiter , Saturn , Venus ila kwa sayari kama Neptune na Uranius itakubidi uwe na vifaa maalumu kama darubini .

— Moja ya tukio zuri kwa wale wanaojihusisha na ufanyaji chunguzi za anga katika upande wa sayari kwa maana ataweza kupata picha ya sayari hizo tajwa kwa urahisi kabisa .

— Mara baada ya giza kutanda katika baadhi ya maeneo watu wataanza kujionea tukio hili kwa mida tofauti tofauti .

#AstronomyKiswahili


Channel name @Chakushangaza
Channel link t.me/chakushangaza


SAMBAZA MARA NYINGI UWEZAVYO