“Puff nani?” niliuliza.
“Puff Daddy.”
“Puff Daddy?”
“Ndiyo.”
“Ndiye nani huyo?”
“Nitajuaje? Ndivyo nilivyoambiwa na jamaa mmoja.”
Kumbuka Puff Daddy alikuwa mtoto wa gangster mkubwa nchini Marekani, aliogopwa na wengi lakini pia alikuwa na uwezo mkubwa wa kuhakikisha kila anapofanya mauaji ama tukio lolote lile, ilikuwa ni vigumu mno kumtia hatiani.
Sasa bwana labda kama huelewi nini kilitokea baada ya kukamatwa kwake. Hebu tusome kidogo.
Baada ya kukamatwa, akataka kutoa kiasi cha dola milioni 50 kwa ajili ya dhamana, yaani hakutaka kukaa gerezani.
Wakamkatalia.
Hii dhamana ilikuwa ni ya mali. Yaani jumba lake la Miami lenye thamani ya dola milioni 48 na nyumba ya mama yake ambayo nayo ipo Miami.
Alikataliwa.
Hiyo ni according to TMZ.
Pia mbali na hiyo akaomba kama haiwezekani ama haijatosha wamzuie kisafiri, wachukue ndege yake binafsi iliyokuwa imepakiwa huko Los Angeles pia na kuvaa GPS device ili afuatiliwe popote atakapokuwa.
Pia wakakataa.
Wakasema akae selo na baadaye atafikishwa mahakamani na kama atakutwa na hatia, atafungwa gerezani kwa miaka 45.
Sasa hivi ana miaka 54 hivyo akitumikia hiyo atatoka akiwa na miaka 99.
Hii miaka 46 imepatikanaje?
1. Utakatishaji pesa adhabu yake miaka 20.
2. Kusafirisha watu kingono miaka 15.
3. Mengineyo miaka 10.
Twende kimatukio yake na tarehe.
NOVEMBA 17, 2023
Aliyewahi kuwa mpenzi wake, Cassi Ventura alimshtaki kwa kusema aliwahi kumnyanyasa kingono, kumpiga mpaka mahusiano yao yalipotamatika mwaka 2018. Hiyo ilikuwa kabla ya video ile akipigwa kuvuja.
NOVEMBA 23, 2023
Mwanamke aitwaye Joi Dickerson naye akapeleka kesi kwamba aliwahi kunyanyaswa kingono na kupokea kichapo huku akirekodiwa. Hiyo ilitokea mwaka 1991 akiwa na miaka 19.
NOVEMBA 24, 2023
Mwanamke mwingine akajitokeza na kusema aliwahi kunyanyaswa kingono na Diddy, akapigwa yeye na rafiki yake mwaka 1990 ama 1991. Pia wakamfuata kwenye apartment yake na kuendelea kumpiga.
DISEMBA 6, 2023
Diddy akapokea mashtaka mengine kwamba kuna mwanamke amejitokeza na kusema yeye na wanaume wawili wa kundi lake walimbaka mwaka 2003 alipokuwa na miaka 17.
FEBRUARI 26, 2024
Rodney Jones, jamaa aliyemsaidia Diddy kuprodyuzi albamu yake ya mwisho, anadai alileweshwa na kuingiliwa kingono kuanzia Septemba 2022 mpaka Novemba 2023.
MEI 21,2024
Mwanamitindo Crystal McKinney alipeleka kesi na kudai alinyanyaswa kingono na mwanaume huyo katika moja ya maonyesho huko New York. Anasema alinyweshwa pombe na hata kuvutishwa bangi na wanaume huyo akiwa na wenzake. Alipolewa, akachukuliwa na kupelekwa bafuni na Diddy kisha kunlazimisha kunyonya dyudyu yake.
MEI 23,2023
April Lampros mwenye miaka 51 akapeleka mashtaka na kusema alikutana na Diddy mwaka 1994 alipokuwa amehudhuria maonyesho ya nguo. Diddy alimlewesha na kumbaka huku akimuahidi angemuingiza kwenye masuala ya urembo.
JULAI 3, 2024
Adria English, mcheza filamu za ngono anasema Diddy alimtumikisha kingono mwanzoni mwa miaka 2000.
SEPTEMBA 24, 2024
Thalia Graves anasema Diddy na mlinzi wake walimbaka kwenye studio za Bad Boys. Anaendelea kusema kwamba alipewa wine ikiwa na kilevi, alipokunywa, akajisikia kizunguzungu na kulala. Alipoamka akajikuta amevungwa kamba huku wawili hao wakiwa wamembaka vya kutosha.